Warombo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Warombo ni watu wa mkoa wa Kilimanjaro, jamii ya Wachagga.

Lugha zao ni Kiseri na lahaja nyingine za Kichagga, yenye asili ya Kibantu[1]. Warombo wameenea mkoa wote na hutambuana kwa kuelewana katika mazungumzo.

Warombo wanajishugulisha na kilimo, ufugaji, biashara na kazi za ofisini.

Vyakula na vinywaji[hariri | hariri chanzo]

Chakula asili cha Warombo ni kitheri, umberere, mabande, ngolowo, irombwe, ng'ande na mtori. Hata hivyo kwa sasa mtori unaliwa na watu mbalimbali ambao si Wachagga na hupikwa hotelini kama chakula.

Kinywaji cha asili cha Warombo kinaitwa Busa. Hapo zamani Warombo walikuwa wanakunywa busa kipindi wakifanya matambiko mbalimbali, kwani ni kinywaji mahususi kinachotayarishwa ili kitumike wakati wa tambiko. Matambiko ya Warombo hufanyika wakati wowote katika mwaka, pia hufanyika kwa lengo la kumwomba Mungu awasaidie katika mambo mbalimbali. Tambiko hufanyika katika mti maalumu ulioandaliwa kwa ajili hiyo na huoteshwa katika kila kaya kwa ajili ya kutunza mazigira na chakula cha mifugo.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Guthrie, Malcolm (2017-09-22), "II Identifying the Bantu Languages", The Classification of the Bantu Languages bound with Bantu Word Division (Routledge): 6–13, ISBN 978-1-315-10553-6, iliwekwa mnamo 2023-05-27 
Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Warombo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.