Wafiadini wa Lyon

Wafiadini wa Lyon ndio Wakristo wafiadini wa kwanza wa Ufaransa[1].
Ni kwamba mwaka 177 dhuluma ya kaisari Marcus Aurelius dhidi ya Ukristo ilisababisha mauaji makubwa katika mji mkuu wa Gallia, jina lake Lugdunum (siku hizi Lyon).
Kati yao, ni maarufu hasa askofu Potinus wa Lyon na mtumwa bikira Blandina wa Lyon. Wengine ni: Aleksanda, Attalus, Vezi Espagati, Maturus, shemasi Sanctius, padri Zakaria, Makari, Asklibiade, Silvio, Primo, Ulpio, Vitale, Komino, Oktoba, Filomeno, Gemino, Julia, Albina, Grata, Emilia, Potamia, Pompea, Rodana, Biblis, Kwarsya, Materna, Elpis, Pontiko, Isto, Aristeo, Korneli, Zosimo, Tito, Julius, Zotiko, Apoloni, JeminianI, Julia mwingine, Ausona, Emilia mwingine, Iamnika, Pompea mwingine, Domna, Yusta, Trofima na Antonia.
Nusu walikuwa wenyeji, nusu walowezi kutoka Frigia, leo nchini Uturuki.
Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 2 Juni[2].
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Kitabu V, I cha Historia ya Kanisa iliyoandikwa na Eusebi wa Kaisarea, kinapatikana katika site de l'antiquité latine et grecque
- Kitabu I, 49 cha Vitabu vitano vya miujiza kilichoandikwa na Gregori wa Tours, kinapatikana katika site de l'antiquité latine et grecque
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |