Vladimir Mkuu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Vladimir wa Kiev)
Ubatizo wa Vladimir, mchoro wa ukutani wa Viktor Vasnetsov.
Ramani inayoonyesha hali ilivyokuwa mwaka 1015 hivi.

Vladimir Mkuu (958 hivi – 15 Julai 1015) alikuwa mtemi wa Kiev na Novgorod kuanzia mwaka 980 hadi kifo chake.

Mwaka 988 alipokea ubatizo kutoka kwa mapadre wa Kanisa la Bizanti uliofuatwa na ubatizo wa familia na wananchi wa utemi wake aliojitahidi kwa nguvu zote kuwaleta kwenye imani ya Kikristo [1][2].

Tukio hilo liliathiri moja kwa moja utamaduni wa Urusi, Ukraina na Belarus pamoja na historia yote iliyofuata, kwa kuwa Kanisa la Kiorthodoksi liliendelea kuwa dini rasmi katika milki za Kirusi hadi Mapinduzi ya Urusi ya 1917.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Oleg Rapov, Russkaya tserkov v IX–pervoy treti XII veka (The Russian Church from the 9th to the First 3rd of the 12th Century). Moscow, 1988.
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/62700
  3. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.