Tian Shan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Milima ya Asia ya Kati, Tian Shan iko upande wa kaskazini ya beseni ya Taklamakan, njano ni barabara ya hariri.
Kitovu cha Tian Shan.

Tian Shan (inayojulikana pia kama Tengri Tagh au Tengir-sana, [1] kwa maana ya Milima ya mbinguni) ni eneo kubwa la milima lililoko Asia ya Kati. Kilele cha juu kabisa katika Tian Shan ni Jengish Chokusu yenye mita 7,493 juu ya UB. Sehemu ya chini ni mwinamo wa Turpan uliopo mita 154 chini ya usawa wa bahari. [2]

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Safu za Tian Shan hutenganishakaskazini na kusini ya Turkestan, na pia kuenea ndani ya Kazakhstan, Kirgizia, Tajikistan, Uzbekistan na eneo la Xinjiang kaskazini-magharibi mwa China.

Tian Shan iko kaskazini na magharibi mwa Jangwa la Taklamakan na moja kwa moja upande wa kaskazini mwa Bonde la Tarim. Upande wa kusini inakutana na Milima ya Pamir na upande wa kaskazini na mashariki hukutana na Milima ya Altai ya Mongolia .

Milima ya Tian Shan ilivyoonekana kutoka anga la nje kwenye Oktoba 1997, Ziwa la Issyk-Kul likionekana huko Kirgizia upande wa kaskazini.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Ensemble Tengir-Too. Aga Khan Trust for Culture. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-07-05. Iliwekwa mnamo 5 July 2019.
  2. Scheffel, Richard L.; Wernet, Susan J., eds. (1980). Natural Wonders of the World. United States of America: Reader's Digest Association, Inc. pp. 378. ISBN 978-0-89577-087-5. 

Vitabu[hariri | hariri chanzo]

  • The Contemporary Atlas of China. 1988. London: Marshall Editions Ltd. Reprint 1989. Sydney: Collins Publishers Australia.
  • The Times Comprehensive Atlas of the World. Eleventh Edition. 2003. Times Books Group Ltd. London.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tian Shan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.