Milima ya Altai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya safu ya mlima wa Altai.

Milima ya Altai ni safu ya milima katika Asia ya Kati na ya Mashariki. Milima mirefu zadi hufikia kimo cha mita 4,500.

Urusi, China, Mongolia, na Kazakhstan zinakutana katika milima hii, ambayo ni chanzo cha mito ya Irtysh na Ob.

Safu hiyo imeungwa na Milima ya Sayan kwenye kaskazini mashariki ikiishia upande wa kusini mashariki katika Jangwa la Gobi.

Wakazi wa eneo lake si wengi wakiwa mchanganyiko wa Warusi, Wakazakhi, Waaltai na Wamongolia.

Uchumi wa eneo hilo unategemea ufugaji wa ng'ombe, farasi na kondoo, pamoja na kilimo, misitu, na uchimbaji madini.

Sehemu ya safu hiyo imeorodheshwa na UNESCO kama urithi wa dunia.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Milima ya Altai kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.