Somanga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Somanga ni kata ya Wilaya ya Kilwa katika Mkoa wa Lindi, Tanzania. Msimbo wa posta ni 65423.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 18,549 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata hii ilikuwa bado sehemu ya kata ya Kinjumbi[2].

Somanga iko kwenye barabara kuu namba B2 kutoka Dar es Salaam kwenda Lindi - Mtwara.

Bomba la gesi kutoka Songosongo linalopita baharini linafikia bara katika eneo la Somanga likiendelea kutoka hapo hadi Dar es Salaam.[3]. Huku kuna pia kituo cha umeme kinachotumia gesi hiyo na kuzalisha umeme kwa mahitaji ya wilaya ya Kilwa.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz/
  2. Sensa ya 2012, Lindi - Kilwa DC. Jalada kutoka ya awali juu ya 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 2019-04-28.
  3. Songo Songo Gas Development and Power-Generation Project, tovuti ya offshore-technology.com
Kata za Wilaya ya Kilwa - Mkoa wa Lindi - Tanzania

Chumo | Kandawale | Kibata | Kikole | Kinjumbi | Kipatimu | Kiranjeranje | Kivinje | Lihimalyao | Likawage | Mandawa | Masoko | Miguruwe | Mingumbi | Miteja | Mitole | Namayuni | Nanjirinji | Njinjo | Pande | Somanga | Songosongo | Tingi


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Lindi bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Somanga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.