Siro na Yohane

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Siro katika mozaiki ya monasteri ya Hosios Lukas.

Siro na Yohane (alifariki Canopus, 31 Januari 311) ni wafiadini Wakristo wa Aleksandria (Misri) waliokatwa kichwa kwa imani yao.

Walikamatwa walipokwenda kuwatia moyo Teodosia, Teotista, Eudosia na mama yao Atanasia.

Kabla ya hapo, Siro alikuwa mganga, halafu mmonaki.

Habari zao ziliandikwa na patriarki Sofroni wa Yerusalemu.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 31 Januari[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.