Siku ya Bwana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ishara ya Chi Rho ikidokeza ushindi wa Mfufuka, 350 hivi.

Siku ya Bwana (kwa Kigiriki, κυρακή ἡμέρα, "kyurakee eemera"; kwa Kilatini, Dominica dies) ni jina ambalo Wakristo wa lugha mbalimbali wanalitumia kutaja Jumapili.

Jina linapatikana katika kitabu cha mwisho cha Biblia ya Kikristo, Ufunuo (1:10).

Chanzo chake ni kwamba ndiyo siku ya juma ambayo wanasadiki Yesu alifufuka kutoka wafu. Hivyo ndiyo mwanzo wa uumbaji mpya wa vyote katika utukufu wake.

Kwa msingi huo, wengi wao wanaiheshimu kama siku muhimu zaidi kwa ibada zao, hasa kwa adhimisho la ukumbusho wake aliloliagiza akiwa katika karamu ya mwisho.

Ushuhuda wa kwanza wa desturi hiyo unapatikana katika Matendo ya Mitume (20:7).

Katika maandishi ya karne ya 2 BK, kwa mfano yale ya Yustino mfiadini, inaonekana desturi hiyo ilivyokuwa imeenea.

Mwaka 361 desturi hiyo iliagizwa rasmi.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • From Sabbath to Lord's Day: A Biblical, Historical and Theological Investigation, D.A. Carson, editor (Grand Rapids, Mich.: Zondervan, 1982).
  • The Study of Liturgy, Cheslyn Jones, Geoffrey Wainwright, Edward Yarnold, SJ, and Paul Bradshaw, editors (New York, N.Y.:Oxford University Press, 1992), pp. 456–458.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Siku ya Bwana kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.