Shirikisho la Amerika ya Kati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Shirikisho la Amerika ya Kati

Shirikisho la Amerika ya Kati (kihisp.: Confederación de Centroamérica) , pia: Maungano ya majimbo ya Amerika ya Kati (Provincias Unidas del Centro de América) ilikuwa maungano ya maeneo ya Amerika ya Kati tangu 1823 hadi 1838. Likajumlisha nchi tano za Guatemala (pamoja na Belize), El Salvador, Honduras, Nikaragua na Costa Rica.

Kabla ya 1821 nchi hizi zote zilikuwa koloni ya Hispania na sehemu za Jimbo Kuu la Guatemala chini ya ufalme mdogo wa Hispania Mpya. Wakati wa kuasi kwa koloni za Hispania katika Amerika jimbo kuu la Guatemala likajiunga na nchi mpya ya Meksiko kwa muda mfupi. Baada ya kupinduliwa kwa mtawala wa kwanza wa Meksiko Agustin de Iturbide jimbo kuu la Guatemala likaamua kuwa nchi ya pekee.

Shirikisho la Amerika ya Kati likaanzishwa mwaka 1823 na mji mkuu ulikuwa Guatemala City. Nchi mpya ilikuwa na matatizo mengi. Mawasiliano yalikuwa magumu kutokana na ukosefu wa barabara. Viongozi wa kila sehemu walitafuta mambo yao bila kujali hali ya shirikisho. Hofu ya kipaumbele cha Guatemala ilisababisha uhamisho wa mji mkuu kwenda El Salvador mwaka 1831.

Jamhuri likaporomoka katika vita ya wenyewe kwa wenyewe tangu 1838. Nikaragua ikajiondoa katika shirikisho tar. 30 Aprili 1838, Honduras ikafuata 26 Oktoba na Costa Rica tar. 14 Novemba 1838. Guatemala ikaondoka 1839 na El Salvador ikabaki pekee yake hadi kufuta jina la shirikisho mwaka 1841.

Majaribo yote ya kuunganisha tena nchi za Amerika ya Kati yalishindikana.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Shirikisho la Amerika ya Kati kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.