Severo wa Napoli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Severo ikitembezwa nyuma ya ile ya Mt. Severino.

Severo wa Napoli (alifariki Napoli, Italia, 29 Aprili 409) alikuwa askofu wa 10 wa mji huo kuanzia Februari 363.

Anasifiwa kwa juhudi zake za kutetea imani sahihi dhidi ya Waario pamoja na rafiki yake Ambrosi wa Milano aliyemuandikia barua[1]. Alipendwa naye kama ndugu, na kupendwa na waumini wake kama baba.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Aprili[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.