Sarah Carneson

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sarah Carneson, (17 Juni, 191630 Oktoba, 2015) alikuwa mratibu wa wafanyakazi wa Afrika Kusini na mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi.

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Sarah Rubin alizaliwa mnamo 1916, huko Johannesburg, binti wa wahamiaji wa Kiyahudi wa Ulaya Mashariki Zelic Rubin (fundi cherehani) na Anna Rubin. Wazazi wake walikuwa miongoni mwa waanzilishi wa chama cha Communist Party nchini Afrika Kusini, na Rubin alipokua mdogo alijiunga na Ligi ya Vijana ya Kikomunisti akiwa kama kijana. [1]

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Sarah Rubin alifanya kazi katika ofisi za Chama cha Kikomunisti huko Johannesburg, kama mwanamke kijana, na alikuwa mwanachama wa Ligi dhidi ya Ufashisti na Vita. Alifundisha madarasa ya kusoma na kuandika kwa wafanyikazi, na alifanya kazi katika duka la vitabu la chama, huko Johannesburg. Kuanzia 1936 hadi 1940, alijihusisha na upangaji wa wafanyikazi, na wafanyikazi wa tumbaku na wafanyikazi wa sukari huko Durban . Mnamo 1945, alikua katibu mkuu wa Jumuiya ya Reli na Bandari ya Afrika Kusini, iliyoko Cape Town. [2]

Sarah na mumewe wote walipigwa marufuku kutoka kwa mikusanyiko ya watu chini ya sheria ya Kukandamiza Ukomunisti (Suppression of Communism Act) ya 1950. Kuendelea kwake kujihusisha na Chama cha Kikomunisti kulipelekea Fred Carneson kukamatwa na kuhukumiwa mnamo mwaka 1956. Sarah Carneson pia aliwekwa kizuizini, mwaka 1960, na kuachiliwa kwa msamaha ili kubaki, chini ya usimamizi, huko Cape Town. Fred alifungwa gerezani mwaka 1965, na Sarah akaondoka Afrika Kusini na kuelekea Uingereza mwaka 1968. Huko Uingereza aliendelea kufanya kazi katika vyama vya wafanyikazi, na katika gazeti la Morning Star . Akina Carneson waliunganishwa tena mwaka 1972, wakiwa uhamishoni huko London. Wenzi hao walirudi Afrika Kusini mnamo mwaka 1991. [3]

Maisha binafsi[hariri | hariri chanzo]

Sarah Rubin aliolewa na Fred Carneson mnamo mwaka 1943, alipokuwa bado kazini katika Vita vya Pili vya Dunia. Walikuwa na watoto watatu, Lynn, John, na Ruth. Sarah alikuwa mjane Fred Carneson alipofariki mwaka 2000. [4] Alifariki mnamo 2015, akiwa na umri wa miaka 99, huko Muizenberg, Cape Town. [5] "Tukio la kumbukumbu ya kitaifa" lilifanyika Cape Town, na kuhudhuriwa na viongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Afrika Kusini, African National Congress, na Cosatu . [6]

Binti yao Lynn alichapisha wasifu wa Carnesons, Red in the Rainbow: Maisha na Nyakati za Fred na Sarah Carneson (2011). Kulipokuwa na maonyesho yanayohusiana kuhusu Carnesons, pia yenye jina la "Red in the Rainbow", katika Jumba la Makumbusho la Slave Lodge(Slave Lodge Museum) mwaka 2015. [7]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Sarah Carneson" South African History Online (2011).
  2. Shaun de Waal, "Sarah Carneson: A lifetime dedicated to SA's freedom struggle" Mail & Guardian (15 November 2015).
  3. "Liberation Hero and Ex-Star Worker Sarah Carneson Dies" Archived 2 Septemba 2017 at the Wayback Machine. People's Daily Morning Star (6 November 2015).
  4. Denis Herbstein, "Fred Carneson" The Guardian (18 September 2000).
  5. Chris Barron, "Obituary: Sarah Carneson, feisty communist harassed and exiled for her beliefs" Sunday Times (8 November 2015).
  6. Carla Bernardo, "SACP’s Sarah Carneson remembered" IOL (5 December 2015).
  7. "RIP Sarah Carneson" Archived 11 Mei 2020 at the Wayback Machine. Iziko Museums of South Africa (3 November 2015).