Salif Keïta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Salif Keita
Taarifa za awali
Amezaliwa25 Agosti 1949 (1949-08-25) (umri 74)
Kazi yakeMwimbaji

Salif Keïta (amezaliwa 25 Agosti 1949) ametambuliwa kimataifa kama mwimbaji wa muziki aina ya afro-pop na mtunzi kutoka Mali. Yeye ni mtu wa kipekee sio kwa sababu tu ya sifa zake kama Sauti ya dhahabu ya Afrika, lakini pia kwa sababu yeye ana uzeruzeru na ana ukoo moja ya mwanzilishi wa himaya ya Mali, Sundiata Keita. Hii ilimaanisha kwamba urithi wake wa kifalme chini ya mfumo wa tabaka wa Mali, hakupaswa kamwe kuwa mwimbaji, ambayo ilikuwa ni jukumu la wengine.

Keita alizaliwa katika mji wa Djoliba. Akatupwa na familia yake na jamii kwa sababu ya uzeruzeru wake, iliyochukuliwa kama ishara ya bahati mbaya katika utamaduni wa Mandinka.[1] Alitoka Djoliba kuelekea Bamako mwaka 1967, ambapo yeye alijiunga na bendi iliyodhaminiwa na serikali iitwayo Super Rail Band de Bamako. Mwaka 1973 Keita alijiunga na kundi, Les Ambassadeurs. Keita na Les Ambassadeurs walikimbia kutoka nchini kwa sababu za rabsh za kisiasa nchini Mali wakati wa miaka ya 1970 hadi Abidjan, Cote d'Ivoire na hatimaye walibadilisha jina la kundi lao kuwa les Les Ambassadeurs internationales. Sifa ya Les Ambassadeurs internationales ilivuma hadi wakajulikana kimataifa katika miaka ya 1970 na mwaka 1977 Keita alipokea Tuzo la Taifa kutoka rais wa Guinea, Sékou Toure.

Keita alihamia Paris mwaka 1984 ili kufikia watazamaji zaidi. Muziki wake huchanganya mitindo ya Afrika Magharibi iliyo na namna kutoka nchi za Ulaya na Amerika, huku akidumisha mtindo wa jumla wa Kiislamu. Vyombo vya muziki ambavyo hupatikana kwa bendi yake ni kama balafon, djembe, gitaa, koras, viungo, saksafoni, na utayarishaji.

Keita alipata mafanikio katika Ulaya kama mmoja wa nyota za Afrika katika dunia ya muziki, lakini kazi yake mara kwa mara nyingine ilikosolewa kwa sababu ya uzalishaji wake duni na kwa ajili ya namna isiyoeleweka. Hata hivyo, muda mfupi baada ya Milenia alirudi Bamako nchini Mali kuishi na kurekodi. Kazi yake ya kwanza baada ya kurejea nyumbani, ilikuwa ni Moffou mwaka 2002, iliyosifiwa kama albamu bora yake katika miaka mingi, na Keita alihamasishwa kujenga studio ya kurekodi katika Bamako, ambayo alitumia kuttayarisha albamu yake, M'Bemba hiyo, iliyotolewa mwezi Oktoba 2005.

Diskografia[hariri | hariri chanzo]

Makusanyiko mengi yanapatikana pia [2] [3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Profaili ya msanii - Salif Keita Archived 24 Machi 2006 at the Wayback Machine.
  2. Salif Keita Discografia
  3. Imekusanywa na Graeme Counsel, Radio Africa, ilipatikana 2009/04/20

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Salif Keïta kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.