Nenda kwa yaliyomo

Rais wa Ujerumani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Rais wa Ujerumani
Frank-Walter Steinmeier

Rais wa Ujerumani ni mkuu wa dola katika Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani.

Kazi yake ni kuwa alama ya umoja wa taifa, lakini katika mfumo wa serikali ya kibunge nchini Ujerumani hana madaraka mengi. Madaraka muhimu ya kisiasa ni kama yafuatayo

  • rais anapaswa kutia sahihi kwa kila sheria iliyopitishwa bungeni. Hapa anaweza kukataa akiona sababu muhimu ya kwamba sheria hailingani na katiba. Akikataa bunge ina njia ya kusahihisha sheria au kumshtaki ais mbele ya mahakama kuu. Tangu 1949 maraisi wa Ujerumani walikataa mara 9 kutia sahihi wakalazimisha serikali na bunge kubadilisha sheria.
  • rais anaamua kama bunge inavunjwa baada ya chansella kushindwa katika swali la imani katika serikali; chansella kama kiongozi wa serikali anaweza kudai kura ya bunge kama ina imani katika serikali. Kama swali hili linakataliwa na wabunge wengi chansella anaweza kumwomba rais kuvunja bunge na uchaguzi wa bunge jipya. Lakini azimio liko mkononi mwa rais anayeweza kumteua kiongozi wingine kuunda serikali mpya.

Rais huchaguliwa kila baada ya miaka 5 na mkutano wa shirikisho (Bundesversammlung) ambao ni wabunge wote pamoja na idadi sawa ya wawakilishi wa mabunge ya majimbo.

Mshahara wa rais ni asilimia 90 za mshahara wa chansella wa Ujerumani. Katika mwaka 2010 hii ililingana na Euro 199,000; pamoja na hayo anapata Euro 78.000 marupurupu ya kando na kwa pesa hii analipa mishahara ya watumishi wa nyumba yake anayopata bure.

Orodha ya marais wa Ujerumani

[hariri | hariri chanzo]

Marais wa Jamhuri ya Weimar (Reichspräsident) (1919-1933)

[hariri | hariri chanzo]
# Picha Jina
(miaka ya maisha)
Tarehe ya kuanza Tarehe ya kwisha Chama
1Friedrich Ebert
(1871-1925)
11 Februari 191928 Februari 1925SPD
2Paul von Hindenburg
(1847-1934)
12 Mei 19252 Agosti 1934-
Adolf Hitler
(1889-1945)
2 Agosti 193430 Aprili 1945NSDAP
3Karl Dönitz
(1891-1980)
30 Aprili 194523 Mei 1945-

Marais wa Ujerumani ya Magharibi (1949–1990)

[hariri | hariri chanzo]
# Picha Jina
(miaka ya maisha)
Tarehe ya kuanza Tarehe ya kwisha Chama
1Theodor Heuss
(1884-1963)
13 Septemba 194912 Septemba 1959FDP
2Heinrich Lübke
(1894-1972)
13 Septemba 195930 Juni 1969CDU
3Gustav Heinemann
(1899-1976)
1 Julai 196930 Juni 1974SPD
4Walter Scheel
(1919-2016)
1 Julai 197430 Juni 1979FDP
5Karl Carstens
(1914-1992)
1 Julai 197930 Juni 1984CDU
6Richard von Weizsäcker
(1920-2015)
1 Julai 198430 Juni 1994CDU

Marais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani (Präsident der Volkskammer)

[hariri | hariri chanzo]
# Picha Jina
(miaka ya maisha)
Tarehe ya kuanza Tarehe ya kwisha Chama
Wilhelm Pieck
(1876-1960)
11 Oktoba 19497 Septemba 1960SED
1Walter Ulbricht
(1893-1973)
12 Septemba 19601 Agosti 1973SED
2Willi Stoph
(1914-1999)
3 Oktoba 197329 Oktoba 1976SED
3Erich Honecker
(1912-1994)
29 Oktoba 197618 Oktoba 1989SED
4Egon Krenz
(1937-)
18 Oktoba 19896 Desemba 1989SED
5Manfred Gerlach
(1928-2011)
6 Desemba 19895 Aprili 1990LDPD
Sabine Bergmann-Pohl
(1946-)
5 Aprili 19902 Oktoba 1990CDU

Marais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani (Bundespräsident) (1990-sasa)

[hariri | hariri chanzo]
# Picha Jina
(miaka ya maisha)
Tarehe ya kuanza Tarehe ya kwisha Chama
6Richard von Weizsäcker
(1920-2015)
since
1 Julai 1984
30 Juni 1994CDU
7Roman Herzog
(1934-2017)
1 Julai 199430 Juni 1999CDU
8Johannes Rau
(1931-2006)
1 Julai 199930 Juni 2004SPD
9Horst Köhler
(1943-2025)
1 Julai 200431 Mei 2010CDU
10Christian Wulff
(1959-)
2 Julai 201017 Februari 2012CDU
11Joachim Gauck
(1940-)
18 Machi 201218 Machi 2017-
12Frank-Walter Steinmeier
(1956-)
19 Machi 2017sasaSPD

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]