Queen Sendiga

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Queen Sendiga
Amezaliwa1973
UtaifaMtanzania
Majina mengineQueen Cuthbert Sendiga
Kazi yakeMwanasiasa, Mwanaharakati, Mfanyabiashara, Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Chama cha siasaAlliance for Democratic Change
MwenzaManeno Mbegu (m. 2013–present) «start: (2013)»"Marriage: Maneno Mbegu to Queen Sendiga" Location: (linkback://sw.wikipedia.org/wiki/Queen_Sendiga)
Watoto3

Queen Cuthbert Sendiga (amezaliwa Rondo, mkoa wa Lindi 1973) ni mwanasiasa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa tangu Mei, 2021. Pia ni mwanaharakati na mfanyabiashara nchini Tanzania.

Ni Naibu Katibu Taifa wa chama cha Alliance for Democratic Change (ADC). Mwaka 2020, Queen aliwahi kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho. [1]

Maisha yake[hariri | hariri chanzo]

Queen Sendiga ni mkazi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Kazi zake[hariri | hariri chanzo]

Queen katika siasa alikuwa mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM mpaka mwaka 2014 alipoamua kuhama na kujiunga na chama cha Alliance for Democratic Change (ADC). Mwaka 2015 kwenye uchaguzi mkuu Tanzania aliwania nafasi ya ubunge jimbo la Kawe kupitika chama cha ADC ila hakufanikiwa kushinda.

Mwaka 2020 kwenye chaguzi za Tanzania alichaguliwa na chama chake cha ADC kuwania nafasi ya urais Tanzania, wakiwa wanawake wawili kupitia vyama vya upinzani na Cecilia Mwanga wa chama cha Demokrasia Makini [2] [3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Queen Sendiga kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.