Modesti wa Yerusalemu

Modesti wa Yerusalemu (Sivas, Kapadokia, leo nchini Uturuki, karne ya 6 – 17 Desemba 630[1]) alikuwa askofu wa mji huo nchini Israeli.
Kabla ya hapo aliuzwa kama mtumwa kwenda Misri. Huko alimuongoa bwana wake ambaye alimuacha huru. Hapo alijiunga na umonaki kwenye mlima Sinai. Baada ya kufanywa abati wa monasteri huko Palestina.
Mwaka 614 Kosroe II wa Persia aliteketeza Yerusalemu akiua Wakristo 66,509. Modesti alichaguliwa kushika nafasi ya askofu Zakaria aliyetekwa, na huyo alipofariki Modesti akawa askofu. Alijitahidi kujenga upya monasteri na makanisa[2].
Tangu kale ametambuliwa kuwa mtakatifu.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 17 Desemba[3].
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Antiochus Strategos, The Capture of Jerusalem by the Persians in 614 AD, F.C. CONYBEARE, English Historical Review 25 (1910) pp. 502-517
- ↑ Archived copy.
- ↑ Martyrologium Romanum
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Building projects of Modestus
- Orthodox Church in America - Modestus of Jerusalem
- Modestus of Jerusalem. Iliwekwa mnamo 6 January 2019.
- St Modestus, Patriarch of Jerusalem. Commemorated December 18 (Civil Date: December 31 ). Iliwekwa mnamo 6 January 2019.
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |