Mgongo kati wa Bahari Hindi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Mgongo Kati wa Bahari Hindi.

Mgongo kati wa Bahari Hindi (kwa Kiingereza: Central Indian Ridge) ni safu ya milima chini ya maji ya Bahari Hindi yenye mwelekeo kutoka kusini hadi kaskazini.

Mpangilio wa kijiolojia[hariri | hariri chanzo]

Sawa na migongo mingine kati ya bahari huo umetokea pale ambako mabamba ya gandunia yaani mapande ya ganda la Dunia hukutana chini ya bahari. Kwenye mstari ambako mabamba hayo yanakutana kuna ufa unaoruhusu kupanda juu kwa magma na lava kutoka koti ya Dunia kama mstari wa volkeno chini ya maji. Miamba hiyo kwenye hali ya kiowevu inaganda inapotoka nje na kuingia katika maji ya bahari, hivyo kujenga safu ndefu ya milima.

Mgongo kati ya Bahari Hindi unatenganisha Bamba la Afrika na mabamba ya Uhindi na Australia.

Mabamba hayo yanatawanya kwenye mgongo kati wa Bahari Hindi yakiachana kila mwaka mnamo milimita 30-50.[1]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Hellebrand et al. 2002, Geological setting, pp. 2306-2308

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vingine[hariri | hariri chanzo]


Coordinates: 34°39′20″S 54°28′58″E / 34.6555°S 54.4828°E / -34.6555; 54.4828