Darfur Magharibi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Magharibi Darfur)

Coordinates: 12°53′N 22°58′E / 12.883°N 22.967°E / 12.883; 22.967

Ramani ya Darfur Magharibi

Darfur Magharibi (Gharb Darfor) ni mojawapo ya majimbo 18 yanayounda Sudan, na moja ya tatu yanayojumuisha kanda ya Darfur. Ina eneo la km² 79,460 na idadi ya wakazi wake inakadiriwa kuwa 1,007,000 (2006).

Inapakana na Darfur Kaskazini na Darfur Kusini upande wa mashariki.

Maeneo ya Chad, Biltine na Ouaddaï yako upande wa magharibi, na upande wa kaskazini kuna mkoa wa Bourkou-Ennedi-Tibesti.

Al-Junaynah ndio mji mkuu wa jimbo hili.

Darfur Magharibi imekuwa eneo kuu la mgogoro wa Darfur unaoendelea.

Makala hii kuhusu maeneo ya Sudan bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Darfur Magharibi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.