Wamaori

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Māori people)
Te Puni, chifu wa Wamaori wa karne ya 19.

Wamaori (kwa kimaori Māori) ni wakazi asilia wa Nyuzilandi. Walikuwa ndio watu wa kwanza kufika kwenye visiwa hivyo.

Mababu zao walikuwa watu wa Polynesia waliofika Nyuzilandi kati ya mwaka 800 na 1300 BK. Katika mapokeo ya Wamaori, mahali wanakotokea huitwa Hawaiki ila haijulikani iko wapi. Neno hilo lina asili moja na neno 'Savaiʻi' la Kisamoa na 'Hawaiʻi' la Kihawaii. Hivyo hakuna uhakika walipotokea, maana wataalamu wanajadiliana kwa kutaja Visiwa vya Cook au visiwa vilivyopo sasa Polynesia ya Kifaransa kama Tahiti.

Katika lugha yao, "Māori" inamaanisha "kawaida". Waliwaita watu wengine, haswa wale waliokuja kutoka Uingereza, "Pākehā". Leo katika Kiingereza cha Nyuzilandi "Pākehā" hutumiwa mara nyingi kama jina la Wazungu wa Nyuzilandi.

Leo wako takriban Wamaori 600,000 wanaoishi Nyuzilandi. Wao ni sehemu muhimu ya utamaduni wa nchi. Hii ndiyo sababu ya kwamba wamepokea haki maalum kutoka kwa serikali ya Nyuzilandi. Lugha yao ya asili, lugha ya Kimaori, ni lugha rasmi ya nchi hiyo pamoja na Kiingereza na Lugha ya Ishara ya Nyuzilandi.

Tovuti za nje[hariri | hariri chanzo]