Lameki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lameki akimuua Kaini (kushoto) kadiri ya hadithi fulani iliyochongwa na Wiligelmo huko Modena (Italia).

Lameki ni jina la watu wawili wa Agano la Kale katika Biblia.

Kitabu cha Mwanzo katika 4:18-24 kinamtaja mmojawao kama mwana wa Metusala katika kizazi cha tano baada ya Kaini. Ndiye wa kwanza kuoa mitara akiwa na wake wawili, Ada e Zila, waliomzalia watoto wanne: Jabal, Jubal, Tubalkain na Naama (huyo wa mwisho akiwa mwanamke). Kila mmojawao anawakilisha fani fulani: uchungaji, muziki, uhunzi na labda umalaya.

Lameki anakumbukwa pia kama mtu wa kisasi kikali.

Kitabu hichohicho kinamtaja Lameki mwingine katika 5:28, mwana wa Metusala katika kizazi cha saba baada ya Seti. Ndiye baba wa Nuhu.