Kusini kwa Sahara

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kusini mwa Sahara)
Hali ya hewa barani Afrika: Kusini kwa Sahara kwanza kuna Sahel na Pembe la Afrika upande wa kaskazini (njano), halafu savana (kijani kibichi) na misitu ya tropiki (kijani iliyokolea) katika Afrika ya Ikweta, hatimaye jangwa la Kalahari (njano) na hali ya Kimediteranea upande wa kusini (rangi ya zeituni) Kusini mwa Afrika. Namba zinaonyesha tarehe za vifaa vya Zama za chuma kuhusiana na uenezi wa Bantu.

Kusini kwa Sahara (mara nyingi Kusini mwa Sahara) ni eneo lote la bara la Afrika ambalo liko upande wa kusini wa Jangwa la Sahara.

Kulingana na Umoja wa Mataifa, eneo hili linajumuisha nchi zote za Afrika ambazo ziko kusini mwa Sahara. Eneo hili linatofautiana na Afrika Kaskazini, ambayo maeneo yake ni sehemu ya Umoja wa Kiarabu.

Somalia, Djibouti, Comoros na Mauritania kijiografia ziko katika Afrika Kusini mwa Sahara, lakini pia zinahesabiwa kuwa sehemu ya dunia ya Kiarabu.

Sahel ni eneo mpito kati ya Sahara na tropiki ya Sudan na kusini zaidi, kwenye misitu ya tropiki-savana.

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kusini kwa Sahara kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.