Kunene (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Maporomoko yaEpupa
Mto Kunene karibu na maporomoko ya Epupa

Kunene (au Cunene) ni mto wa Afrika ya kusini-magharibi.

Chanzo chake kiko Angola katika Nyanda za Juu za Bie, unaelekea kusini hadi kufikia mpaka wa Namibia kwenye mji wa Ruacana.

Kuanzia hapo mto ni mpaka kati ya Angola na Namibia hadi kufikia bahari ya Atlantiki. Mdomo wa mto baharini ni delta yenye upana wa km 30.

Mwendo wote ni wa km 1207, beseni lina km² 109,832 .

Kunene ina maporomoko huko Ruacana, pia Epupa.

Serikali ya Namibia ilipanga kutengeneza lambo kwenye maporomoko ya Epupa. Mipango hii imepingwa vikali kwa sababu inaonekana kuhatarisha ekolojia ya eneo pamoja na hali ya maisha ya Wahima walio wenyeji.

Jina la mto unarudia katika jina la mkoa wa Namibia wa Kunene.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kunene (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.