Kunegunda wa Luxemburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Kunegunda alivyochorwa na Master of Meßkirch, 1535/1540, Staatsgalerie Stuttgart.

Kunegunda wa Luxembourg, OSB (975 hivi – Kaufungen, 3 Machi 1040[1]) alikuwa mke wa kaisari wa Dola Takatifu la Kiroma (Ujerumani) Henri II[2][3].

Inasemekana waliishi bila kufanya tendo la ndoa[4][5] na waligawa mali nyingi kwa watu fukara na kufadhili Kanisa kwa namna mbalimbali.

Mwaka mmoja baada ya kufiwa mume wake, aliingia monasterini na kumfanya Kristo kuwa urithi wake kama alivyotamani tangu ujanani.

Alipofariki yeye pia, alizikwa kwa heshima zote karibu na mumewe.

Tarehe 29 Machi 1200 alitangazwa na Papa Innocent III kuwa mtakatifu, kama mumewe.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Machi[6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Martyrologium Romanum, 3 March, #8 (2005)
  2. "Saint Kunigunde". New Catholic Dictionary. saints.sqpn.com. 7 October 2012.  Check date values in: |date= (help)
  3. http://www.santiebeati.it/dettaglio/43700
  4. "St. Cunegundes, Empress - Pictorial Lives of the Saints: with Reflections for Every Day in the Year". Garden of Mary. 
  5. Farmer, David Hugh (1997). The Oxford dictionary of saints (toleo la 4.). Oxford [u.a.]: Oxford Univ. Press. ku. 119. ISBN 0-19-280058-2. 
  6. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.