Kolosai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Magofu ya Kolosai.

Kolosai (kwa Kigiriki Κολοσσαί, Kolosai), ulikuwa mji wa mkoa wa Frigia (katika Uturuki wa leo) juu ya mto Lukus, kilometa 22 kusini kwa Laodikea, karibu na barabara kutoka Efeso hadi mto Eufrate.

Umaarufu wake unatokana na barua ambayo Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo wa huko, waliokuwa wamehubiriwa Injili na mwanafunzi wake Epafra, mwenyeji wa huko[1], lakini waliaanza kupokea mafundisho tofauti yaliyoonekana na Paulo kuwa ya kizushi kwa kuwa yalipunguza umuhimu wa Yesu Kristo.

Barua hiyo imeingizwa katika Agano Jipya la Biblia ya Kikristo kwa jina la Waraka kwa Wakolosai.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Easton's Bible Dictionary, 1897.
  • Bennett, Andrew Lloyd. "Archaeology From Art: Investigating Colossae and the Miracle of the Archangel Michael at Kona." Near East Archaeological Society Bulletin 50 (2005):15-26.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Coordinates: 37°47′16.18″N 29°15′41.55″E / 37.7878278°N 29.2615417°E / 37.7878278; 29.2615417