Epafra
Mandhari

Epafra (kwa Kigiriki Ἐπαφράς, Epafras; alifariki Kolosai, 80) alikuwa mwanafunzi na msaidizi wa Mtume Paulo katika uinjilishaji wa mji wa Efeso na mkoa wa Asia.
Inaonekana alikuwa mwenyeji wa Kolosai na alitumwa kueneza Ukristo huko (Kol 1:7; 4;12-13) pamoja na Laodikea na Yerapoli.
Baada ya muda, yalijitokeza huko matatizo ya kiimani yaliyomfanya Paulo aandike barua maarufu kama Waraka kwa Wakolosai.
Paulo anamtaja pia kama mfungwa mwenzake (Waraka kwa Filemoni 1:23).
Kwa jinsi alivyomsifu, kama mshiriki mpenzi wa kazi yake na mtumishi mwaminifu wa Kristo, tangu kale anaheshimiwa na madhehebu mengi kama mtakatifu[1].
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Mabradha wa Shule za Kikristo
- Orodha ya Watakatifu Waaugustino
- Orodha ya Watakatifu Wabazili
- Orodha ya Watakatifu Wabenedikto
- Orodha ya Watakatifu Wadominiko
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Watakatifu Wajesuiti
- Orodha ya Watakatifu Wakarmeli
- Orodha ya Watakatifu Wakolumbani
- Orodha ya Watakatifu Wamersedari
- Orodha ya Watakatifu Waoratori
- Orodha ya Watakatifu Wapasionisti
- Orodha ya Watakatifu Wapremontree
- Orodha ya Watakatifu Waredentori
- Orodha ya Watakatifu Wasalesiani
- Orodha ya Watakatifu Waskolopi
- Orodha ya Watakatifu Wateatini
- Orodha ya Watakatifu Watrinitari
- Orodha ya Watakatifu Watumishi wa Maria
- Orodha ya Watakatifu Wavinsenti
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Epafra kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |