Kisiwa cha Mainland
Mandhari


Mainland ndicho kisiwa kikuu cha funguvisiwa la Shetland, upande wa kaskazini ya Uskoti (Scotland). Inahesabiwa kuwa sehemu ya Uskoti.
Visiwa vya Shetland viko baharini kati ya Visiwa vya Faroe na Visiwa vya Orkney. Funguvisiwa hilo liko mpakani kati ya Bahari Atlantiki upande wa magharibi na Bahari ya Kaskazini upande wa mashariki.
Kwa jumla kuna visiwa 100 na kati yake 16 vinakaliwa na watu 23,510[1]. Eneo lote ni km² 1,426 na theluthi mbili zake ni eneo la kisiwa cha Mainland. Makao makuu ya utawala na mji mkubwa ni Lerwick.
Tabianchi ni nusu aktiki na si baridi sana kutokana na athira ya mkondo wa ghuba.
Uchumi
[hariri | hariri chanzo]Uchumi wa visiwa unategemea kilimo na hasa ufugaji wa kondoo.
Mwaka 1969 mafuta ya petroli yaligunduliwa yakawa chanzo kipya cha mapato.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kisiwa cha Mainland kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |