Kibwirosagi
Mandhari
| Kibwirosagi | ||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kibwirosagi kichwa-cheusi | ||||||||||||||
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
| Ngazi za chini | ||||||||||||||
|
Jenasi 7 na spishi 9 za vibwirosagi:
|
Vibwirosagi ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Cisticolidae. Wanafanana na videnenda lakini mkia wao ni mrefu zaidi na wana rangi kali zaidi: nyekundu, kijani, kahawia na/au kijivu mgongoni na njano, nyekundu, marungi, hudhurungi na/au kijivu chini. Wanatokea Afrika kusini kwa Sahara katika misitu na mapori. Hula wadudu. Hulijenga tago lenye kuba ya manyasi, majani na/au vigoga katika kichaka, mmea au dege la watoto. Jike huyataga mayai 1-4.
Spishi
[hariri | hariri chanzo]- Bathmocercus cerviniventris, Kibwirosagi Tumbo-hudhurungi (Black-Headed Rufous Warbler)
- Bathmocercus rufus, Kibwirosagi Uso-mweusi (Black-Faced Rufous Warbler)
- Eminia lepida, Kibwirosagi Utosi-kijivu (Grey-capped Warbler)
- Euryptila subcinnamomea, Kibwirosagi Kidari-marungi (Kopje au Cinnamon-breasted Warbler)
- Hypergerus atriceps, Kibwirosagi Kichwa-cheusi (Oriole Warbler)
- Incana incana, Kibwirosagi wa Sokotra (Socotra Warbler)
- Malcorus pectoralis, Kibwirosagi Masikio-mekundu (Rufous-eared Warbler)
- Scepomycter rubehoensis, Kibwirosagi wa Rubeho (Rubeho Warbler)
- Scepomycter winifredae, Kibwirosagi wa Uluguru (Winifred's au Mrs. Moreau's Warbler)
Picha
[hariri | hariri chanzo]- Kibwirosagi uso-mweusi
- Kibwirosagi utosi-kijivu
- Kibwirosagi kidari-marungi
- Kibwirosagi wa Sokotra
- Kibwirosagi masikio-mekundu