Kidenenda

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kidenenda
Kidenenda mvivu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Cisticolidae (Ndege walio na mnasaba na videnenda)
Sundevall, 1872
Ngazi za chini

Jenasi 2:

Videnenda ni ndege wadogo wa jenasi Cisticola na Incana katika familia Cisticolidae. Chimbuko la jenasi lipo Afrika lakini spishi kadhaa zinatokea Ulaya na Asia pia, spishi moja hata mpaka Australia. Ndege hawa hupatikana kwa maeneo wazi, k.m. savana, jangwa, mbuga na mabwawa. Rangi yao kuu ni kahawia mara nyingi pamoja na michirizi mizito na pengine nyekundu au njano. Hula wadudu. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe ndani ya uoto mzito; mara nyingi tago limefunika na manyasi yaliyofumika. Jike huyataga mayai 3-5.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Spishi ya Asia na Australia[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]