Hassi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Hassium)


Hassi (hassium)
Jina la Elementi Hassi (hassium)
Alama Hs
Namba atomia 108
Mfululizo safu Metali ya mpito
Uzani atomia 265, 269, 270
Valensi 2, 8, 18, 32, 32, 14, 2
Densiti 41 g/cm³ (kadirio)
Ugumu (Mohs) (haijulikani)
Asilimia za ganda la dunia 0 % (elementi sintetiki)
Hali maada inaaminiwa ni mango
Mengineyo tamburania, nururifu

Hassi (hassium) ni elementi ya kikemia iliyo na alama Hs na namba atomia 108. Hassi ni yenye dutu nururifu; isotopi iliyo thabiti zaidi ni 269 Hs, ikiwa na nusumaisha ya takriban sekunde 16.

Hassi ni elementi sintetiki ambayo haipatikani kiasili; inaweza kutengenezwa kwa viwango vidogo kwenye maabara.

Majaribio ya kwanza ya kusanidi elementi 108 zilifanywa katika maabara ya Dubna, Moscow Oblast, kwenye Umoja wa Kisovyeti, mnamo 1978. Hatimaye wanasayansi katika taasisi ya utafiti wa ioni nzito huko Darmstadt, Ujerumani, waliweza kuonyesha kwamba walifaulu kuitengeneza.

Kwa hiyo wanasayansi Wajerumani walipewa nafasi ya kuchagua jina la elementi mpya wakachagua jina hassium kutokana na Hesse, moja ya majimbo 16 ya shirikisho la Ujerumani.

Hakuna habari nyingi kuhusu tabia za Hessi maana inaweza kutengenezwa tu kwenye maabara kwa viwango vya gramu lakini kwa gharama kubwa, na baada ya kutengenezwa haidumu maana atomu zake zinaachana haraka.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Kujisomea[hariri | hariri chanzo]