Fosyo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Mt. Fosyo Mkuu katika ukuta wa kanisa kuu la Mt. Sofia, Kiev (Ukraina).

Fosyo (kwa Kigiriki: Φώτιος, Fōtios[1]; Konstantinopoli (leo nchini Uturuki), 810/820Bordi, Armenia, 6 Februari 893) alikuwa Patriarki wa Konstantinopoli miaka 858-867 halafu 877-886;[2] Kwa ujuzi wake mkubwa[3] na kwa umuhimu wake katika historia ya Kanisa, Waorthodoksi wanamuita Fosyo Mkuu[4].

Farakano la muda la miaka 863-867 kati ya Kanisa la Roma na lile la Konstantinopoli kuhusu upatriarki wa Fosyo lilikuwa baya kuliko yote kabla ya farakano la mwaka 1054 ambalo limedumu hadi leo kati ya Ukristo wa Magharibi na Waorthodoksi.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi kwama mtakatifu[5], ingawa alitangazwa rasmi mwaka 1847 tu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Fr. Justin Taylor, essay "Canon Law in the Age of the Fathers" (published in Jordan Hite, T.O.R., & Daniel J. Ward, O.S.B., "Readings, Cases, Materials in Canon Law: A Textbook for Ministerial Students, Revised Edition" [Collegeville, MN: The Liturgical Press, 1990]), p. 61
  2. White, Despina Stratoudaki. The Life of Patriarch Photios. Patriarch Photios of Constantinople, His Life, Scholarly Contributions, and Correspondence, Together with a Translation of Fifty-two of His Letters. Iliwekwa mnamo 2014-01-03.
  3. Louth 2007, Chapter Seven: "Renaissance of Learning: East and West", p. 159; Mango 1980, p. 168.
  4. Photius the Great, Patriarch of Constantinople. Online Chapel. The Greek Orthodox Archdiocese of America. Iliwekwa mnamo 10 June 2016.
  5. И. Византийский. Святѣйшій Фотій, патріархъ Константинопольскій (The Most Holy Photius, Patriarch of Constantinople) // «Церковныя Вѣдомости, издаваемыя при Святѣйшемъ Правительствующемъ Сѵнодѣ» («Ecclesiastical leaflets of the Most Holy Governing Synod»). 29 January 1900, № 5, pages 193—201.

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.