Fake Pastors

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Fake Pastors

Posta ya Fake Pastors
Imeongozwa na Gervas Kasiga
Imetayarishwa na Eric Shigongo
Imetungwa na Eric Shigongo
Gervas Kasiga (muswada andishi)
Nyota Adam Kuambiana
Vicent Kigosi
Jokette Mwegelo
Lisa Jensen
Blandina Changula
Emmanuel Myamba
Imetolewa tar. 3 Aprili, 2007
Ina muda wa dk. 120
Nchi Tanzania
Lugha Kiswahili

'Fake Pastors ni jina la filamu iliyotoka mwaka 2007 kutoka nchini Tanzania. Washiriki wakuu ni Adam Kuambiana (Petro), Vicent Kigosi (Ray), Jokette Mwegelo (Jach), Lisa Jensen (Lisa), na Blandina Chagula. Filamu hii imeandikwa (muswada) na kuongozwa na Gervas Kasiga na kutayarishwa na Eric Shigongo na Kigosi. Filamu inahusu wachungaji wawili wanaotumia shida za waumini wao kama sehemu ya mtaji wa kuwataka aidha kimapenzi au kifedha. Filamu inaonyesha tabia za baadhi ya wachungaji bandia waliokithiri katika ulimwengu wetu. Filamu hii ni moja ya filamu zilizopata sifa kubwa katika filamu za Tanzania. [1] Filamu imetengenezwa na Doroth Kipeja na kampuni yake ya Tripod Media.

Hadithi[hariri | hariri chanzo]

Filamu inaanza na vijana wawili watanashati Patrick (Vicent Kigosi) na Petro (Adam Kuambiana) waliohitumu Chuo Kikuu cha Mzumbe, Morogoro. Akilini mwao wanaelewa kitu kimoja tu walichoambiwa tangu utotoni kuwa ukiwa na shahada maisha yatakuwa rahisi jambo ambalo baada ya kuingia mitaani wanakuta ni tofauti kwani hakuna ajira na maisha yanakuwa magumu sana kwao.

Baada ya kutembea katika ofisi moja hadi nyingine wakitafuta kazi bila mafanikio, hatimaye wanagundua kuanzisha kanisa ndio suluhisho pekee walilobakiza. Hivyo wanaamua kuwa wachungaji wa bandia (Fake Pastors). Dhima ya kuanzisha kanisa ilikuwa ni kujitajirisha badala ya kumtumikia Mungu, kazi yao inakuwa ni kuwakamua waumini fedha na mali walizonazo.

Kwakufanya hivyo wanajikusanyia utajiri mkubwa hasa baada ya misada kuanzia kuingia kutoka nje kwa wahisani, baadala ya kufanya kazi ya Mungu wao wanazitumia fedha hizo katika anasa wakilewa pombe na malaya na ifikapo asubuhi wanahubiri injili kama kawaida na kuwafanya waumini wazidi kuwaamini. Baadaye walijiingiza katika biashara haramu dawa za kulevya ndipo hapo bahati yao ilipoenda kombo na kuanguka vibaya katika hila zao.

Washiriki[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Fake Pastors kama waigizaji wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.