Eusebi wa Samosata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu wa Mt. Eusebi.

Eusebi wa Samosata (alifariki Dolikha, leo Dülük, Uturuki, 379 hivi) alikuwa askofu wa Samosata kuanzia mwaka 361 hadi kifodini chake.

Alidhulumiwa na Dola la Roma kwa kupinga Uario ulioungwa mkono na makaisari. Chini ya Konstanti II aliimarisha waumini wake katika imani sahihi kwa kuwatembelea huku amevaa kama askari, halafu chini ya Valens alipelekwa uhamishoni huko Thrakia [1][2].

Hatimaye, kisha kupatikana tena amani kwa Kanisa Katoliki chini ya Theodosi Mkuu, aliuawa na mwanamke wa madhehebu hayo aliyemrushia kigae kichwani[3][4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 22 Juni[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.