Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture, kifupi: TCCIA) ni shirika lisilo la serikali linalounganisha wanachama ambao ni makampuni na wajasiriamali nchini Tanzania.

Shabaha yake ni kuendeleza maslahi ya wanachama wake na sekta binafsi ya uchumi kwa jumla. Inalenga kurahisisha uhusiano kati ya sekta binafsi na sekta ya umma nchini na kuwasilisha maslahi ya sekta binafsi mbele ya serikali.

TCCIA ilianzishwa mnamo mwaka 1988 na ofisi kuu zake zipo katika mkoa wa Dar es Salaam. Ilichukua jukumu kubwa katika ubinafsishaji wa makampuni ya umma ya awali na uhuru wa uchumi Tanzania.[1]

Uendeshaji[hariri | hariri chanzo]

TCCIA imefungua matawi katika mikoa 21 na vituo 92 nchini kwenye ngazi ya wilaya nchini Tanzania, kwa kushirikiana na SIDA (Shirika la Ushirikiano wa Maendeleo la Kimataifa la Uswidi).

TCCIA kwa sasa ina wanachama zaidi ya 9,000 na ilianzisha mtandao wa shirika na vyama vya hiari, pamoja na uhusiano na Shirikisho la Wajasiriamali Wanawake wa Tanzania. Haya ni maendeleo mazuri kwani mashirika hayo mawili yana malengo yanayokamilika. TCCIA inachukua faida ya mtandao kupitia maneno "peke yako wewe ni dhaifu, pamoja tuna nguvu".

Huduma zinazotolewa na TCCIA kwa jamii ya wafanyabiashara ni pamoja na habari za biashara, mafunzo, utetezi, mipango ya kusaidia biashara (kama vile usindikaji na leseni ya biashara na shughuli za kukuza biashara, kwa mfano, programu za uuzaji, maonyesho ya biashara na misheni.

Chemba ya Biashara inapokea idadi kubwa ya maswali ya biashara kutoka kote ulimwenguni. Yanayohusu kampuni zinazojaribu kupata wateja au wauzaji na zinachapishwa kwenye jarida, na kusambazwa kwenye makampuni yote ya wanachama waliomaliza kulipa.

Shirika[hariri | hariri chanzo]

Halmashauri ya biashara na sekta ya uchumi ni pamoja na:[2]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Archived copy". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-08-28. Iliwekwa mnamo 2008-12-24.  Unknown parameter |url-status= ignored (help)
  2. ""Committee", archived copy". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-12-04. Iliwekwa mnamo 2008-12-24.  Unknown parameter |url-status= ignored (help)