Chawa
Chawa | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Chawa wa kichwa (Pediculus humanus capitis)
| ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||
Familia za juu 4: |
Chawa ni wadudu wadogo wa oda ndogo Phthiraptera katika nusuoda Troctomorpha wa oda Psocodea. Wahenga wao ni chawa-vitabu na kama hawa chawa hawana mabawa. Wadudu hawa wote ni vidusia wa nje juu ya ndege na mamalia isipokuwa Monotremata (kinyamadege na mhanganungu), popo, nyangumi, pomboo na kakakuona. Kuna aina mbili za chawa: wanaokula nywele, manyoya na seli za ngozi zilizokufa, na wanaofyunza damu ya mwenyeji. Chawa wa aina ya kwanza wana vipande vya mdomo vya kutafuna, wale wengine wana mdomo wa kufyunza. Miguu inabeba aina za magando madogo ili kushika nywele au manyoya ya mwenyeji. Kwa kawaida mayai ya chawa yamegandia nywele au manyoya, au pengine yamewekwa ndani ya shina la unyoya.
Uharibifu wa chawa na jinsi ya kumuangamiza[hariri | hariri chanzo]
Chawa wanaopatikana kichwani hawana magonjwa yoyote wanayosababisha lakini waliye mwilini huwa wanasababisha magonjwa. Hata hivyo, katika jamii nyingi, chawa huonekana kana kwamba huwasumbua walio wachafu ama wanaoishi kwa uchafu. Pia hufanya mtu adhoofike kwa sababu ya kunyonywa na vidusia hawa.
Kuna dawa kadhaa za kupuliza ili kuwaua wadudu hawa. Usafi pia ni muhimu kama wataka kuwakwepa.
Picha[hariri | hariri chanzo]
-
Amblycera (Menacanthus stramineus)
-
Amblycera (Menacanthus sp.)
-
Anoplura (chawa wa mbeleni, Pthirus pubis)
-
Anoplura (yai la chawa wa mbeleni)
-
Anoplura (chawa wa ngagi, Pthirus gorillae)
-
Ischnocera (chawa wa njiwa, Columbicola columbae)
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
![]() |
Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Chawa kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |