Clatous Chama

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Chama Clatous)

Clatous Chama, (wakati mwingine huripotiwa kama Cletus Chama; alizaliwa 18 Juni 1991) ni mchezaji wa soka wa Zambia.

Chama aliisaidia ZESCO United F.C. kufika nusu fainali za Ligi ya Mabingwa ya CAF kabla ya kusaini mkataba wa miaka 3 na Al Ittihad ya Misri.

Hata hivyo, mwezi wa Februari 2017 Chama aliichezea Lusaka Dynamos F.C. kabla ya kujiunga na klabu ya Simba S.C. iliyopo nchini Tanzania mwaka 2018 kwa kusaini mkataba wa miaka miwili.

Mwaka 2019 Chama aliongeza mkataba wa miaka 2 hadi mwaka 2022 lakini mwaka 2021 alisajiliwa na klabu ya RS Berkane ya Moroko kwa mkataba wa miaka mitatu. Baada ya kuitumikia Berkane kwa muda mchache alirejea katika klabu yake ya awali Simba s.c na alipata mafanikio kwa kuifikisha timu robo fainali kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika. Chama ameisaidia Simba kutwaa ligi kuu, ngao ya jamii na sasa wanawania ubingwa wa VPL

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Clatous Chama kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.