Azam Media Limited

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Azam Media Limited ni kampuni ya burudani na mawasiliano inayotoa huduma za televisheni, redio, na mtandaoni.

Azam Media inajulikana kwa huduma zake za televisheni za kulipia ambazo zinajumuisha chaneli za runinga za ndani na za kimataifa, pamoja na huduma za on-demand na vipindi vya michezo.

Kampuni pia inaendesha vituo vya redio na inatoa huduma za mtandaoni kupitia programu yake ya Azam TV.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Ilianzishwa nchini Tanzania na Sheikh Said Salim Bakhresa mnamo mwaka 2013.

Azam Media imekuwa ikiongeza wigo wake katika nyanja mbalimbali za burudani na mawasiliano nchini Tanzania na kwingineko.[1]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Azam Media Limited kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.