Atala wa Bobbio

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Atala.

Atala wa Bobbio (Burgundy, karne ya 6 - Bobbio, Italia, 10 Machi 627) alikuwa mmonaki kutoka Ufaransa wa leo anayejulikana hasa kama mfuasi wa Kolumbani huko Luxeuil, alipohamia kutoka monasteri ya Lerins ili kupata maisha magumu zaidi.

Baada ya kufukuzwa nchini (612), walianzisha monasteri mpya huko Bobbio (614) ambayo baada ya mwaka mmoja ilibaki chini yake kutokana na kifo cha Kolumbani (615).

Aliongoza kwa ari na utambuzi hivi kwamba chini yake monasteri hiyo ikastawi sana pamoja na kuvuta Walombardi Waario katika Kanisa Katoliki[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 10 Machi[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Giona di Bobbio, Vita Sancti Columbani et discipulorum eius, Francia 642 circa.
  • Dio è corazza dei forti. Testi del cristianesimo celtico (VI-X sec.), Rimini, Il Cerchio, 1998.
  • Archivum Bobiense, Rivista annuale degli Archivi storici Bobiensi (1979-2008), Bobbio
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.