Ufalme wa Bizanti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ufalme wa Byzanti)
Mabadiliko ya eneo la Bizanti au Roma ya Mashariki

Ufalme wa Bizanti (kwa Kigiriki: Βυζαντινή Αυτοκρατορία) ni neno linalotumika kutaja Dola la Roma lilivyoendelea mashariki mwa eneo la kandokando ya bahari ya Mediteranea katika Zama za Kati, ukiwa na makao yake makuu kwenye mji wa Konstantinopoli (ulioitwa pia Bizanti) na kutumia lugha ya Kigiriki.

Katika baadhi ya maana, hasa baada ya kuanguka kwa Dola la Roma Magharibi na mjini Roma penyewe, hujulikana pia kama Dola la Roma Mashariki.

Wabizanti wenyewe walijiona ni bado Dola la Roma likiendelea tu. Watawala walitumia cheo cha "Kaisari" kama awali.

Hata hivyo, kwa wakati mwingi wa historia yake, ulifahamika na wenzao wa Ulaya magharibi kama “Ufalme wa Wagiriki” au “Ufalme wa Konstantinopoli” au "Rhômania".

Lakini majirani wa mashariki kama Waarabu waliendela kuwaita "Waroma" (kwa Kiarabu روم rum).

Bizanti ilipata mapigo mawili makubwa katika historia yake:

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ufalme wa Bizanti kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.