Nasaba ya Tang

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya China wakati wa nasaba ya kifalme ya Tang. Rangi ya njano inaonyesha China yenyewe na rangi ya njano-nyeusi ni maeneo yaliyokuwa chini ya China wakati ule
Kitabu cha Kibuddha kilikuwa kitabu cha kwanza duniani kilichochapishwa kwa wingi mnamo mwaka 868

Nasaba ya Tang (Kichina: 唐朝; Pinyin: Táng Cháo) ilikuwa nasaba ya kifalme iliyotawala nchi ya China kuanzia mwaka 618 hadi 907 BK.

Kipindi cha Tang inahesabiwa kati ya sehemu bora ya historia ya China. Mji mkuu wa Chang'an (leo hii Xi'an) ilikuwa mji mkubwa wa dunia wakati wake ukiwa na wakazi wapatao milioni 1. Milki ya Tang ilisimamia sehemu kubwa ya barabara ya hariri na kwa njia wageni wengi walifika China. Wakati wa Tang siasa na jamii ya Kichina ilikuwa tayari kupokea wageni na kuishi nao. Hali hii ilisaidia maendeleo ya kiutamaduni. Wakati ule Ubuddha ulienea China. Vilevile wamisionari Wakristo wa kwanza walifika kutoka Uajemi wakakaribishwa na watawala.

Uchumi ulipanuka pamoja na miji. Mifereji ilichimbwa na kuwa njia za mawasiliano na kusafirisha bidhaa na mazao. Migodi zaidi ya 150 ilipeleka madini wa matumizi katika uchumi wa milki.

Sanaa mbalimbali zilistawi kama vile uchoraji, fasihi, muziki. Ufinyanzi ulifikia kiwango bora. Utawala uliboreshwa kwa kuwagawia ardhi wakulima wadogo, sheria kali mno zilifutwa na mfumo wa kodi kuboreshwa.

Kati ya teknolojia zilizobuniwa na kuanzishwa wakati wa Tang ni

Wataalamu wa China wakati ule waligundua mkia wa nyotamkia na kutambua ugonjwa wa usukari.

Nguvu ya milki iliiwezesha kupanusha utawala wake juu ya maeneo makubwa ya Asia ya Mashariki na ya Kati. Katika upanuzi huo viongozi wa kijeshi waliongezeka umuhimu wakaanza kushindana kati yao. Wakubwa wa jeshi na dola walitwaa maeneo makubwa zaidi kama mali ya binafsi na tabaka ya wakulima wadogo iliharibika wakashuka chini kuwa wafanyakazi watupu mashambani. Hayo yote yalisababisha ghasia na vita ya wenyewe kwa wenyewe. Mwishoni mtawala wa mwisho wa Tang alipinduliwa na jenerali wa jeshi alikamata utawala akaua watoto wote wa nasaba ya kifalme.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]


Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Kujisomea[hariri | hariri chanzo]

  • Charles Benn: China's Golden Age. Everyday Life in the Tang Dynasty. Oxford University Press, New York/NY 2004, ISBN 0-19-517665-0.
  • Peter K. Bol: “This Culture of Ours.” Intellectual Transitions in T'ang and Sung China. Stanford University Press, Stanford/CA 1992, ISBN 0-8047-1920-9.
  • Otto Franke: Geschichte des chinesischen Reiches. Band 2. De Gruyter, Berlin/Leipzig 1936.
  • Charles Hartmann: Han Yü and the T'ang Search for Unity. Princeton University Press, Princeton/NJ 1986.
  • Dieter Kuhn (Hrsg.): Chinas Goldenes Zeitalter. Die Tang-Dynastie (618–907 n. Chr.) und das kulturelle Erbe der Seidenstraße. Edition Braus, Heidelberg 1993, ISBN 3-89466-069-4.
  • Mark Edward Lewis: China's Cosmopolitan Empire. The Tang Dynasty. Belknap, London/Cambridge (Massachusetts) 2009.
  • Colin Mackerras: The Uighur Empire according to the T'ang dynastic Histories. A Study in Sino-Uighur Relations 744-840. Canberra 1972
  • David McMullen: State and Scholars in T'ang China. Cambridge University Press, Cambridge 1988, ISBN 0-521-32991-4.
  • Stephen Owen: The Great Age of Chinese Poetry. The High T'ang. Yale University Press, New Haven 1981, ISBN 0-300-02367-7.
  • Denis C. Twitchett: Financial Administration under the T'ang Dynasty. 2. Auflage. Cambridge University Press, Cambridge 1970, ISBN 0-521-07823-7.
  • Denis C. Twitchett: The Writing of Official History under the T'ang. Cambridge University Press, Cambridge 1992, ISBN 0-521-41348-6.
  • Denis C. Twitchett, John K. Fairbank (Hrsg.): The Cambridge History of China, Vol. 3. Sui and T'ang China, 589–906. Cambridge University Press, Cambridge 1979, ISBN 0-521-21446-7.
  • Arthur F. Wright, Denis C. Twitchett (Hrsg.): Perspectives on the T'ang. Yale University Press, New Haven 1973, ISBN 0-300-02674-9.
  • Howard Wechsler: Offerings of Jade and Silk. Ritual and Symbol in the Legitimation of the T'ang Dynasty. Yale University Press, New Haven 1985, ISBN 0-300-03191-2.
  • Stanley Weinstein: Buddhism under the T'ang. Cambridge University Press, Cambridge 1987, ISBN 0-521-25585-6.
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nasaba ya Tang kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.