Panagia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Panagia kutoka Yaroslavl, karne ya 13.

Panagia (kutoka Kigiriki: Παναγία, Mtakatifu kabisa) ni jina la heshima kwa Bikira Maria, mama wa Yesu, linalotumika hasa katika Ukristo wa Mashariki. Linasisitiza utakatifu wake uliozidi ule wa binadamu wengine wote, isipokuwa Mwanae.

Jina hilo linatumika pia kwa aina maalumu ya picha takatifu za Mama wa Mungu zinazomuonyesha akisali huko akimuelekea mtazamaji kama uso kwa uso na kuwa na Mwanae amechorwa katika duara kifuani mwake[1].

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Great Panagia, History of Russian Painting, by Boguslawski

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • The Blackwell Dictionary of Eastern Christianity, p. 368 (ISBN|0-631-23203-6)