Kulala kwa Mama wa Mungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya fumbo hilo iliyochorwa na msanii wa Novgorod, Urusi.

Kulala kwa Mama wa Mungu ni sikukuu ya Kanisa ambayo ni maarufu katika Ukristo wa mashariki, yaani Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki na Makanisa Katoliki ya Mashariki vilevile.

Inaadhimishwa kila mwaka tarehe 15 Agosti baada ya wiki mbili za mfungo.

Inalingana na sherehe ya Maria kupalizwa mbinguni inayofanywa na Kanisa la magharibi siku hiyohiyo.

Neno "kulala" linachukuliwa kwa maana ya "kufa" kabla ya "kufufuliwa" na "kuchukuliwa mbinguni" kwa mwili wake.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kulala kwa Mama wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.