Narsisi wa Yerusalemu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Narsisi katika dirisha la kioo cha rangi.

Narsisi wa Yerusalemu (99 - 216) alikuwa askofu wa 30 wa Yerusalemu, uliokuwa umejengwa upya kama mji wa Kipagani, kuanzia uzee mkubwa hadi kifo chake, ingawa katikati alikwenda kuishi upwekeni na nafasi yake ikashikwa na maaskofu wengine watatu[1].

Alisaidia kufanya Wakristo wa Palestina wakubali kuadhimisha Pasaka siku ya Jumapili kila mwaka, kwa kuwa ndiyo siku ya ufufuko wa Yesu.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Oktoba[2] au 7 Agosti.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Rev. Hugo Hoever; S.O.Cist., wahariri (1955). Lives of the Saints, For Every Day of the Year. New York: Catholic Book Publishing Co. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.