Kolmani wa Dromore

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kolmani wa Dromore (pia: Mocholmóc; alifariki karne ya 6) alikuwa abati[1][2][3] wa monasteri aliyoianzisha huko Dromore[4], halafu pia askofu wa mji huo[5] katika kisiwa cha Ireland. Alijitahidi sana kueneza imani ya Kikristo katika eneo la Down[6].

Pengine anachanganywa na Kolmani mwingine aliyekuwa askofu katika Visiwa vya Orkney huko Uskoti na kufariki mwaka 1010 hivi[7][8].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu. Papa Leo XIII alithibitisha heshima hiyo tarehe 19 Juni 1902[9].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Juni[10].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Filippo Caraffa e Giuseppe Morelli (curr.), Bibliotheca Sanctorum (BSS), 12 voll., Istituto Giovanni XXIII nella Pontificia Università Lateranense, Roma 1961-1969. (Kiitalia)
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.