Akko

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Akko kutoka juu.

Akko (kwa Kiebrania: עַכּוֹ, ʻAkkō; pia: Akka (kwa Kiarabu: عكّا, ʻAkkā[1]; uliwahi kuitwa pia: Tolemais) ni mji wa pwani katika Israeli Kaskazini. Una bandari asili katika Hori ya Haifa.[2]

Kutokana na umuhimu wa mahali ulipo, umekaliwa na watu mfululizo tangu zama za Shaba hadi leo,[3] ingawa uliwahi kuangamizwa mara kadhaa.

Wakazi wa sasa ni 48,000 hivi.

Mwaka 58 Mtume Paulo alikaa siku moja na Wakristo wa huko mwishoni mwa safari yake ya tatu ya kimisionari, akielekea Yerusalemu (Mdo 21:7)

Umeorodheshwa na UNESCO kati ya mahali pa Urithi wa Dunia.

Ni pia makao makuu ya dini ya Bahai.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Acre: Historical overview Archived 1 Septemba 2018 at the Wayback Machine. (Hebrew)
  2. "Old City of Acre.", UNESCO World Heritage Center. World Heritage Convention. Web. 15 Apr 2013
  3. Petersen, 2001, p. 68

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Akko travel guide kutoka Wikisafiri

Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Akko kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.