Wafiadini wa Mar Saba (20 Machi)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Monasteri ya Mar Saba kutoka juu.

Wafiadini wa Mar Saba (20 Machi) (walifia dini katika monasteri ya Mar Saba, leo nchini Palestina, 797) walikuwa wamonaki Wakristo 20 waliouawa na Waislamu kwa ajili ya imani yao.

Walikufa kwa kukosa hewa kutokana na moshi wa moto uliowashwa katika kanisa la Mama wa Mungu.

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 20 Machi[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.