Ugonjwa wa akili

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wanawake wanane wakiwakilisha maradhi ya akili yalivyotambulikana katika karne ya 19 huko Salpêtrière (Paris, Ufaransa). Mchoro wa Armand Gautier.

Ugonjwa wa akili ni tabia ya kuwaza na kutenda namna ambayo ama inasababisha mateso ama walau haifai kukabili maisha halisi.[1] Namna hiyo inaweza kuwa ya kudumu, au kujitokeza mara moja tu au kwa kwikwi au kurudi tena baada ya kuonekana imekwisha.

Aina nyingi za ugonjwa wa akili zimefafanuliwa na kuorodheshwa, kila moja ikiwa na dalili zake za pekee.[2]

Sababu za ugonjwa mara nyingi hazieleweki. Nadharia zinaweza kutegemea utafiti wa aina tofautitofauti. Kwa kawaida ugonjwa wa akili unaelezwa kuchangiwa na jinsi mtu anavyohemka, anavyotenda, anavyowaza na anavyohisi watu, vitu na matukio.[2] Hiyo inaweza kuwa na chanzo katika sehemu fulani ya ubongo, na katika maisha ya kijamii. Fani inayochunguza maradhi hayo inaitwa saikopatolojia.

Huduma kwa wenye ugonjwa wa akili zinatolewa katika hospitali maalumu au katika jumuia chini ya madaktari wa akili, wanasaikolojia na wanasosholojia, wanaotumia mbinu mbalimbali, hasa kutazama na kuuliza maswali. Dawa zinatolewa kadiri ya maagizo ya madaktari hao.[2]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Stein, Dan J. (December 2013). "What is a mental disorder? A perspective from cognitive-affective science" (PDF). Canadian Journal of Psychiatry 58 (12): 656–62. PMID 24331284. Archived from the original on 2016-03-04. Retrieved 2016-02-03. 
  2. 2.0 2.1 2.2 Mental disorders Fact sheet N°396. World Health Organisation (October 2014). Iliwekwa mnamo 13 May 2015.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Atkinson, J. (2006) Private and Public Protection: Civil Mental Health Legislation, Edinburgh, Dunedin Academic Press ISBN 1-903765-61-7
  • Hockenbury, Don and Sandy (2004). Discovering Psychology. Worth Publishers. ISBN 0-7167-5704-4. 
  • Fried, Yehuda and Joseph Agassi, (1976). Paranoia: A Study in Diagnosis. Boston Studies in the Philosophy of Science, 50. ISBN 90-277-0704-9. 
  • Fried, Yehuda and Joseph Agassi, (1983). Psychiatry as Medicine. The Hague, Nijhoff. ISBN 90-247-2837-1. 
  • Porter, Roy (2002). Madness: a brief history. Oxford [Oxfordshire]: Oxford University Press. ISBN 0-19-280266-6. 
  • Weller M.P.I. and Eysenck M. The Scientific Basis of Psychiatry, W.B. Saunders, London, Philadelphia, Toronto etc. 1992
  • Wiencke, Markus (2006) Schizophrenie als Ergebnis von Wechselwirkungen: Georg Simmels Individualitätskonzept in der Klinischen Psychologie. In David Kim (ed.), Georg Simmel in Translation: Interdisciplinary Border-Crossings in Culture and Modernity (pp. 123–155). Cambridge Scholars Press, Cambridge, ISBN 1-84718-060-4

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ugonjwa wa akili kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.