Teresa Eustoki Verzeri

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Teresa Verzeri.

Teresa Eustoki Verzeri (Bergamo, Lombardia, 31 Julai 1801Brescia, 3 Machi 1852) alikuwa mwanamke wa Italia kaskazini ambaye, baada ya kuacha monasteri ya Wabenedikto, alianzisha shirika la Mabinti wa Moyo Mtakatifu wa Yesu kwa ajili ya kulea wasichana. Jina lake la awali lilikuwa Ignazia[1].

Alitangazwa mwenye heri na Papa Pius XII tarehe 27 Oktoba 1946, halafu mtakatifu na Papa Yohane Paulo II tarehe 10 Juni 2001[2].

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe ya kifo chake[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.