Steve Bruce

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Steve Bruce

Stephen Roger Bruce (alizaliwa Disemba 31, 1960) ni mchezaji na kocha wa mchezo wa mpira wa miguu. Alicheza soka katika nafasi ya beki wa kati na aliwahi kuchezea vilabu mbalimbali vya soka kama vile Norwich city na Manchester united.

Bruce pia alipata mafanikio makubwa alipokuwa na klabu ya Manchester united ambapo alishinda mataji yapatayo 12 huku matatu yakiwa ni ya Ligi ya Uingereza, matatu ya kombe la FA na kadharika. japokuwa na mafanikio yake yote hakuwahi kuchaguliwa kucheza katika timu yake ya taifa. wachambuzi wa soka wamesema kuwa yeye ni mchezaji bora wa Uingereza kati ya miaka ya 1980s hadi 1990s.

Bruce alianza kazi yake ya ukocha na klabu ya Sheffield United, na baadaye kutumia mda kidogo na klabu za Huddersfield Town, Wigan Athletic na Crystal Palace kabla ya kujiunga na Birmingham City mnamo mwaka 2001.

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Steve alizaliwa huko Corbridge huko Northumberland, ni mzazi wa wana wawili Joe na Sheenagh Bruce. Baba yake alikuwa mtu kutoka ndani ya Uingereza, na mama yake alikuwa amezaliwa Bangor katika kisiwa cha Kaskazini. Familia yao waliishi Daisy Hill karibu na Wallsend, na Bruce alihudhuria Shule ya Benfield.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Steve Bruce kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.