Roderiki na Solomoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Roderiki katika mavazi ya ibada ya padri.

Roderiki na Solomoni (walifariki Cordoba, Hispania, 13 Machi 857) walikuwa watu wa Hispania waliouawa na Waislamu waliotawala nchi hiyo kwa sababu ya imani yao ya Kikristo.

Padri Roderiki alipokataa kusadiki kwamba Muhamadi alikuwa kweli nabii kutoka kwa Mwenyezi Mungu, alitupwa gerezani alipokutana na Solomoni, ambaye alikuwa amewahi kusilimu kwa muda fulani; hatimaye walishinda jaribu lao kwa kukatwa kichwa.[1] na mwingine mwenzake gerezani[2]

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Machi[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Tolan, John, Medieval Christian Perceptions of Islam, New York: Routledge, 2000. ISBN|0-8153-1426-4

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.