Parapela

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Parapela (rafadha) ya eropleni.

Parapela[1] (kutoka Kilatini propellere = kusogeza mbele) ni jina la rafadha ikitumiwa kwenye ndege.

Parapela inatumia fizikia kama kila rafadha inasababisha tofauti ya kanieneo inayovuta ndege mbele.

Helikopta huwa na parapela mbili; parapela kubwa inavuta helikopta juu na parapela ndogo ya nyuma husaidia kupanga mwelekeo wake inapokwenda.

Parapela za ndege hutengenezwa kwa kutumia ubao, plastiki na kwa mashine kubwa metali.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Parapela ni pendekezo la KAST; Kamusi Kuu inataja pia propela kama kisawe cha rafadha