Parapela
Parapela[1] (kutoka Kilatini propellere = kusogeza mbele) ni jina la rafadha ikitumiwa kwenye ndege.
Parapela inatumia fizikia kama kila rafadha inasababisha tofauti ya kanieneo inayovuta ndege mbele.
Helikopta huwa na parapela mbili; parapela kubwa inavuta helikopta juu na parapela ndogo ya nyuma husaidia kupanga mwelekeo wake inapokwenda.
Parapela za ndege hutengenezwa kwa kutumia ubao, plastiki na kwa mashine kubwa metali.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Parapela ni pendekezo la KAST; Kamusi Kuu inataja pia propela kama kisawe cha rafadha