Parapela
Jump to navigation
Jump to search
Parapela (kutoka Kilat. propellere = kusogeza mbele) ni jina la rafadha ikitumiwa kwenye eropleni.
Parapela inatumia fizikia kama kila rafadha inasababisha tofauti ya kanieneo inayovuta ndege mbele.
Helikopta huwa na parapela mbili; parapela kubwa inavuta helikopta juu na parapela ndogo ya nyuma husaidia kulanga mwelekeo wake inapoenda.
Parapela za ndege hutengenezwa kwa kutumia ubao, plastiki na kwa mashine kubwa metali.