Olegari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake.

Olegari (kwa Kikatalunya: Oleguer Bonestruga; Barcelona, 1060 hivi - Barcelona, 1137) alikuwa askofu wa Barcelona na wa Tarragona, nchini Hispania, kuanzia mwaka 1116.

Kabla ya hapo alikuwa mkanoni mwanajimbo, halafu Mwaugustino, halafu abati wa monasteri. Alipochaguliwa kuwa askofu alikataa cheo hicho mpaka alipoagizwa na Papa Paskali II[1].

Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu. Heshima hiyo ilithibitishwa na Papa tarehe 18 Mei 1675.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 6 Machi[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.